Jumanne, 22 Desemba 2020

                     

                      SADAKA NI NINI?


SADAKA NI NINI??????..........................

Kabla ya kuleta somo hili fupi, naweza kusema kuwa Mtazamo wa Madhehebu kila siku ni wa UONGO na UTAPELI.
MTAZAMO WA HUU UKURASA HAUPO KATIKA UPANDE WOWOTE ULE ILA TU KATIKA BIBLIA.
Tuta chambua kwa vipengele vifatavyo
1.SADAKA NI TAMBIKO AU KAFARA
2.SADAKA NI HISANI
3.SADAKA NI UPENDELEO
SADAKA NI NINI?
kwanza kabisa ndugu msomaji unatakiwa utambue kuwa neno SADAKA limetokana na neno lenye asili ya lugha ya kiarabu yaani SADAQAH
.>>>>''Sadaqah 'inamaanisha' haki 'na inahusu utoaji wa hiari wa neema au sadaka. [4] Katika istilahi ya Kiislamu, sadaqah imeelezewa kama kitendo cha "kutoa kitu ... bila kutafuta mbadala kwa kurudi na kwa nia ya kumpendeza Mwenyezi Mungu." [5] Wakati huo huo, kulingana na Ar-Rageeb al-Asfahaani "Sadaqa ndio nini Mtu anatoa kutoka kwa kile alichonacho, kama Zakat, akitazamia kumkaribia Mwenyezi Mungu. "
KATIKA AGANO LA KALE SADAKA ILIMAANISHA NINI?.
-katika AGANO LA KALE sadaka ilimaanisha MATOLEO YA AINA ZOOTE AMBAYO WANA WA ISRAELI waliyotoa kama TORATI ilivyo amrisha kwa ajili ya MATAMBIKO YA IBADA ZAO
UTHIBITISHO WA HAYO MANENO,
8:4 WAEBRANIA
''Kama angekuwa juu ya nchi, asingekuwa kuhani; maana wako watoao SADAKA kama IAGIZAVYO SHERIA''
Huo ulikuwa ni mtazamo wa AGANO LA KALE.
katika Agano Jipya kwa ajili ya Utoaji wa vitu halisi visivyokuwa matoleo au dhabihu.
neno SADAKA halipaswi kutumika kwa maana ile ya kwanza na ya pili ambayo humaanisha TAMBIKO au KAFARA na UPENDELEO la^
Bali neno hilo linapaswa kutumika kama maana ya HISANI(ALMS).Ila neno hili au hilo SADAKA madhehebu mengi duniani hasa wanaotumia lugha ya KISWAHILI yamekuwa wakitumia neno hili au hilo SADAKA kwa maana ya ujumla.
yaani
SADAKA ni jitolea katika HURUMA na UPENDO wa kweli bila SHERIA ya kudai kurudishiwa kile ulicho kitoa,
SADAKA
ni kujitolea katika kuwafadhili wahitaji pasipo ubaguzi wowote ule au kutaka Maslahi ya aina yoyote yale Binafsi ya kuwamiliki wahitaji kupitia SADAKA husika.
SADAKA
ni kitendo cha kujitolea wema kwa IMANI na KUTARAJIA kupata THAWABU zaidi kutoka kwa MUNGU ambaye ndiye mmiliki wa Vitu vyote.
kuna SADAKA ya kuonekana kwa macho ya kibinadamu na isiyoonekana kwa macho ya kibinadamu
USHAHIDI WA KIBIBLIA
14;2 Hosea
'Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie Bwana; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema; na hivyo ndivyo mtakavyotoa sadaka za midomo yetu kana kwamba ni ng'ombe'.
119;108 Zaburi
''Ee Bwana, uziridhie sadaka za kinywa changu, Na kunifundisha hukumu zako.
13;15-16 Waebrania
''15.Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.
16 Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu''
10;1-2 Matendo
''Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,
2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima''.
1,Petro 2;5
''5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo''
Tuna kushukuru saana ndugu msomaji wetu kwa kuwa karibu nasi.
kwa maswali au maoni karibu.
Page yetu haifungamani katika upate wowote ule wa DHEHEBU au DINI,Hii page yenye nia njema juu ya WATU WOOTE....
TUNA WAPENDA UPEO.




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

  Yesu Kama Mwalimu Mkuu (Waebrania 1, Luka 2, Mathayo 13, Luka 16)   Utangulizi: Je, ulipokuwa shule uligundua kuwa baadhi ya walimu waliku...